HISTORY

Hawala:Mashirika ya mis­aada yaonya


Mashirika ya ki­mataifa ya ku­toa mis­aada ya kib­i­nadam, yame­onya kuwa huenda yakalaz­imika kusi­tisha shughuli zao zote nchini So­ma­lia, ikiwa Kenya itabadili ua­muzi wake wa ku­funga vi­tuo vya ku­tuma na kubadil­isha sarafu za ki­geni maarufu kama hawala, ku­fu­a­tia sham­bu­lio lililo­fanywa na wapi­ganaji wa Al shabaab, katika chuo ki­moja kikuu mjini Garissa.

Kwa mu­jibu wa taar­ifa ku­toka kwa mashirika kumi na tano ya mis­aada, mashirika hayo hutu­mia vi­tuo hivyo ku­tuma pesa nchini So­ma­lia na kulipa misha­hara na kodi kwa wafanyakazi wake.

Mashirika hayo yame­sema, ag­izo hilo litakuwa na athari kubwa sana kwa raia masikini wa So­ma­lia, kwa sababu wao hutege­mea fedha wana­zopokea kupi­tia vi­tuo hivyo ku­nunua chakula, kulipa karo na pia ku­pata huduma za afya.

Serikali ya Kenya ime­sema ime­funga vi­tuo hivyo ili kuzuia kundi hilo la Al shabaab kupokea fedha ku­toka kwa wafad­hili wake katika mataifa ya ki­geni.