HABARI KIBAJUNI

Yemen:Serikali hupinga madhungumudho na waasi


Serikali ya Yemen iliyoko uhamishoni, haitakubali kufanya madhungumdho ya amani na vanamgambo wa Houthi, hadi pale vanamgambo hao vatakapotekeledha maafikiano ya baradha la usalama la umoja wa mataifa.

Miongoni wa muafaka huo, ni kuondoka kutoka kachika muyi vanayoshikilia na kurejesha silaha validhotukua.

Hayo yamesemwa leo Jumanne na makamu wa Rais Khaled Bahah.

Shirika la Umoya wa mataifa lilikuwa na tumaini makubwa kuwa makundi dhote hasimu iini Yemen, kwa pamoya na kundi kuu la Houthi na serikali ya Abd-Rabbu Mansour Hadi iliyoko uhamishoni muyini Riyadh, yataungana kwa madhungumudho ya kuetcha amani huko Geneva hatimaye mwedhi huu ili kujaribu kulecha suluhu na kukomesha mapigano dhaliyodumu miedhi kadhaa sasa.