CULTURE

U atapo haki yako


Namba nawe mlimwengu, pulikidha matamko
Nikweledhe neno langu, udhinduwe bongo lako
Nayo nda Mungu si yangu, na ayani haya yako
Uatapo haki yako,  utaingiya mochoni
2
Simama uchechee, usivikhofu vichuko
Aliyo nayo mwendee, akupe kilicho chako
Akipinga mlemee, mwandame kulla endapo
Uatapo haki yako, utaingiya mochoni
3
Amkeni mulolala,na mwenye shikio koko
Isive mcho kulola,nachuchidhame chwendapo
Chuwate na kuduwala,usingidhi si mashiko
Uatapo haki yako,utaingiya mochoni
4
Checheya kwa kula hali, usiche misukosuko
Siche wingi wala mali,sabilisha roho yako
Unyonge usikubali, ukaonewa kwa chako 
Uatapo haki yako, utaingiya mochoni
5
Siche kifaru na ndovu, wangazidi nguvu dhako
Wapempe kwa uwekevu, unusuru haki yako
Siandame vapumbavu,kilicho chako ni chako
Uatapo haki yako, utaingiya mochoni
6
Cha mchu hakifichiki,ikafungiwa ilipo
Hudhuka ikawa hiki,kadhanya utoe chako
Uatapo haki yako,fahamu ni dhara kwako
Leo na kwa Mola wako,utaingiya mochoni