HABARI KIBAJUNI

EU yatakiwa kusaidia chachidho la usafirishaji haramu vahamiaji


Waziri Mkuu wa Italy, Matteo Renzi alisema umoya wa ulaya ladhima usaidie kachika chachidho la kukabiliana na usafirishaji haramu vahamiaji kachika mataifa ya ki-Afrika baada ya wahamiaji vapachao 900 kudhama Jumapili wakati boti yavo ilipodhama kwenye bahari ya Mediterranean.

Bwana Renzi alitoa matamshi hayo Jumatano wakati akidhungumdha na wabunge wa Italy muyini Rome siku moya kabla ya viongodhi wa ulaya kukuchana kwa kikao cha dharura kudhungumudhia machachidho hayo. Wabunge pia waliomboledha kwa kukaa kimwa kuwakumbuka vatchu valiofariki kutokana na ajali hiyo.

Kundi la haki dha binadamu la Save the Children iliripoti Jumatano kwamba ilipacha taarifa kwamba vachocho wadogo wapachao 60 walikuwa ndani ya boti wakati ilipodhama na kundi imevona kwamba kama hali hii ya sasa inaendelea vachocho wahamiaji wasiopungua 2,500 watawedha kufariki kachika ajali kama hidho kwenye bahari ya Mediterranean mwaka huu.

Save the Children indaeleza kwamba wavulana wane ambao vanasema vanaumri tini ya miaka 18 valinusurika kutoka ajali ya Jumapili wakati kapteni wa boti ya vahamiaji hao kwa bahati mbaya alipogonga boti kwenye meli ya midhigo iliyokua inaelekea kuvaokoa.

Waendesha mashtaka wa Italy katika muyi wa Sicilia wa Catania walisema kapteni wa boti hiyo raia wa Tunisia aliongodha boti hiyo iliyoyaa vachu kupicha kiasi hadi meli ya kontena ya Ureno muda mfupi kabla ya kudhama inde ya pwani ya Libya siku ya Jumamosi usiku April 18 mwaka 2015. Maafisa wanasema hiyo ni ajali mbaya kabisa iliyosababisha kifo vengi kuwahi kutokea kachika bahari ya Mediterranean. Kuna vachu 28 pekee valionusurika.

Mwendesha mashtaka ameondowa lawama dhodhote dha uwajibikaji kwa meli hiyo ya midhigo.